MRADI WA MAJI WA Tsh BILIONI 70.5 – UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI

Mhe RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, MHE SAMIA SULUHU HASSAN aliweka JIWE la MSINGI kwenye Mradi wa ujenzi wa BOMBA la MAJI la Mugango-Kiabakari-Butiama utakaogarimu Tsh BILIONI 70.5 – haya ni MAJI ya kutoka Ziwa Victoria

Jumapili, tarehe 6.2.2022, Mhe RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, MHE SAMIA SULUHU HASSAN aliweka JIWE la MSINGI kwenye Mradi wa ujenzi wa BOMBA la MAJI la Mugango-Kiabakari-Butiama utakaogarimu Tsh BILIONI 70.5 – haya ni MAJI ya kutoka Ziwa Victoria.

TUKIO hilo lilifanyika ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini, Kijijini KWIBARA, MUGANGO

VIKUNDI vya KWAYA na NGOMA za ASILI vya Jimboni mwetu vilitoa burudani wakati wa sherehe hizo muhimu sana zikizofanyika Jimboni mwetu.

VIDEO zilizowekwa hapa zimerekodi kwa kifupi sehemu ya burudani ya siku hiyo ya tarehe 6.2.2022. Tafadhali sikiliza na angalia baadhi ya NGOMA za ASILI za Jimbo la Musoma Vijijini.

UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM – UTAMADUNI & MICHEZO

*Kila mwaka, siku ya sherehe za NANENANE, Jimbo letu linafanya MASHINDANO ya Kwaya, Ngoma za Asili na Mitumbwi (kupiga makasia).

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
10.2.2022