UIMARISHAJI WA UTAMADUNI NA MICHEZO NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI.

Na: Wasaidizi wa Mbunge
*Hamisa Gamba
*Fedson Masawa
*Verediana Mgoma
*Vaileth Peter
JIMBO la  Musoma Vijijini lenye KATA 21 zenye VIJIJI 68 na VITONGOJI 374 limeamua kufufua na kuimarisha NGOMA za ASILI, KWAYA na MICHEZO ya aina mbalimbali chini ya ufadhili wa Mbunge wao wa Jimbo, Profesa Sospeter Muhongo.
USHAURI unaotolewa ni wa KILA KATA kuunda VIKUNDI au TIMU za kushindanishwa na KATA nyingine.
*MASHINDANO YA NGOMA ZA ASILI & KWAYA*
*Sherehe za kila mwaka za NANENANE zinatumika kumpata MSINDI wa KWANZA hadi wa TATU kwenye mashindano ya Ngoma za Asili na Kwaya. Mbunge wa Jimbo ndiye mfadhili wa mashindano haya.
*MASHINDANO YA KUPIGA KASIA*
*Jimbo lina jumla ya Vikundi/Timu 18 za kupiga kasia
*Mashindano haya hufanyika kila mwisho wa mwaka kwa WAPIGA KASIA kushindana umbali wa kati ya mita 1,000 na 1,500 ndani ya Ziwa Victoria. Mfadhili wa mashindano haya ni Mbunge wetu wa Jimbo.
*MPIRA WA MIGUU JIMBONI MWETU*
*Jimbo lina TIMU 78 za Mpira wa Miguu. Mashindano ya Mchezo wa Mpira wa Miguu yanafanyika kwa nyakati tofauti tofauti Jimboni mwetu.
*Utaratibu unatengenezwa wa kupata TIMU ya MPIRA ya Jimbo letu ambayo itashiriki Mashindano mbalimbali kwenye ngazi za Wilaya na Mkoa. Mbunge wa Jimbo alishagawa jezi na mipira kwa kila Kata, na hivi karibuni ataanza kugawa tena vifaa hivyo.
*Mbunge wa Jimbo alitoa mchango mkubwa kuipandisha TIMU ya BIASHARA kuingia LIGI KUU ya TAIFA.
*Vilevile, Mbunge wa Jimbo letu alikuwa mfadhili mkuu wa TIMU ya WASAGA (Kijiji cha Kasoma) iliyofanikiwa kuingia FAINALI YA LIGI DARAJA LA PILI ya Mkoa wa Mara.
*ORODHA NA IDADI YA VIKUNDI VYA NGOMA ZA ASILI ni kama ifuatavyo:*
*Jimbo lina Vikundi 27 vilivyogawanyika katika Makundi 5 kama ifuatavyo
*1. DOGOLI* : Vikundi 4
*2. GITAA*  :   Kikundi  1
*3. LIRANDI / LITUNGU* : Vikundi 2
*4. MBEGETE* : Vikundi 3
*5. ZEZE* : Vikundi 2
*IDADI YA KWAYA JIMBO MWETU*
*UIMBAJI ni kipaji cha pekee kwa Wana Musoma Vijijini.
*Karibu kila Kijiji kina kwaya moja au zaidi. KWAYA kuu zinazotambulika ni 15.
KARIBU UFURAHIE UTAMADUNI WA MUSOMA VIJIJINI – ILANI YA UCHAGUZI YA CCM INATEKELEZWA KWA VITENDO KWENYE MAENEO YOTE!