EID EL FITR NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI –  SHEREHE NA MAENDELEO VIJIJINI

Mbunge wa Jimbo akiwa na Waumini wa Dini ya Kiislamu na Wegeni wengine waalikwa kwenye eneo la Sherehe ya Eid el Fitr Kijijini Kome.

I – MASJID KOME
Kijiji cha Kome, Kata ya Bwasi
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo AMEWAKARIBISHA WAISLAMU wa Kijiji cha Kome na kutoka Vijiji jirani KIFUNGUA KINYWA (Eid el Fitr Breakfast) na CHAKULA CHA MCHANA (Eid el Fitr Lunch) kwenye ENEO ambalo MSIKITI wa Kijiji UTAJENGWA.
Wananchi walipata fursa ya kueleza KERO zao ambazo zilijibiwa na Mbunge huyo.
II – CHEMISTRY LABORATORY OF NYANJA SECONDARY SCHOOL
Baada ya kupata KIFUNGUA KINYWA Msikitini, Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo ALIENDA KUKAGUA ujenzi wa MAABARA za Nyanja Secondary School iliyoko hapo Kijijini.
Sekondari ya Kata ya Bwasi (Nyanja Secondary School). Inakamilisha ujenzi wa MAABARA 3 za Chemistry, Physics na Biology. BOMA lenye Vyumba 3 vya Maabara hizo limekamilika. Kinachoendelea kwa sasa ni kuweka MIUNDOMBINU ya ndani ya MAABARA hizo. Wameanza na Maabara ya Kemia (Chemistry Laboratory).
Ujenzi huu unasimamiwa na BODI ya Shule, Mwenyekiti ni Ndugu Abel Bohohe na Mwalimu Mkuu, Mwl Charles Ndebele. Viongozi hawa WACHAPAKAZI WAZURI wamesema kwamba LENGO lao ni kukamilisha Maabara ya Kemia ifikapo tarehe 30.08.2019.
Mbunge Prof Sospeter Muhongo alipokuwa Shuleni hapo alipata fursa ya kuongea na Wanafunzi wanaosoma Masomo ya Sayansi na baadae ALICHANGIA UJENZI huo wa ndani ya Maabara kwa KUNUNUA NONDO 35 zilizokuwa zinahitajika kwa hatua hii ya ujenzi. Nondo zilinunuliwa hapo Kijijini.
Mbunge Prof Muhongo akiwa  Nyanja Secondary School alikagua UJENZI wa MIUNDOMBINU wa Maabara ya KEMIA. Mbunge huyo aliongea na Wanafunzi na baadae akaenda Kijijini kununua NONDO 35 zilizoombwa kwa ajili ya hatua hii ya ujenzi.
Baada ya kushiriki Eid el Fitr Kijijini Kome (Masjid Kome), Mbunge Prof Muhongo aliendelea kuungana na Waislamu wa Misikiti ya Vijiji vya Mayani – Masjid Ququ bin Amri (Kata ya Tegeruka) na Nyegina – Masjid Othman (Kata ya Nyegina).