WANAVIJIJI WA KATA YA KIRIBA – WASEMA – “HAKUNA MTOTO ALIYECHAGULIWA KWENDA FORM I ATAKAYEBAKI NYUMBANI KWA SABABU YA UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SEKONDARI YAO YA KATA.”

Baadhi ya Matukio ya tarehe 31.12.2018 Kijijini Bwai Kwitururu nyumbani kwa Familia ya Prof Muhongo.

Wanafunzi 236 wa Kata ya Kiriba yenye Vijiji 3 wamefaulu na kuchaguliwa kujiunga na Masomo ya Sekondari.
Kutokana na UPUNGUFU MKUBWA wa Vyumba vya Madarasa ni WANAFUNZI 50 tu, watajiunga (07.01.2019) na Masomo ya Sekondari kwenye Sekondari ya Kata ya Kiriba (Kiriba Secondary School).
Wanafunzi 186 WATABAKI NYUMBANI wakisubiri upatikanaji wa Vyumba vya Madarasa kwenye Sekondari ya Kata yao.
UAMUZI WA WANANCHI na VIONGOZI WAO
Tarehe 31.12.2018, wakati wa CHAKULA CHA KUAGA Mwaka (2018) na KUKARIBISHA Mwaka Mpya (2019), Wananchi walitumia fursa hiyo kujadiliana na Mbunge wao Prof Muhongo namna ya KUTATUA TATIZO HILO SUGU LA UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA.
Chakula hicho kilitayarishwa na Familia ya Prof Muhongo ya Kijijini Bwai Kwitururu, Kata ya Kiriba.
Tarehe 01.01.2019, UONGOZI WA KATA uliweka RATIBA YA KAZI YA UJENZI WA VYUMBA 4 VYA MADARASA MAPYA yanayohitajika na kazi ya ujenzi inaanza Jumatatu, tarehe 07.01.2019 na kukamilika tarehe 30.01.2019. Ujenzi ukiaanza KWA UAMUZI na MATAKWA ya WANAVIJIJI wa KATA YA KIRIBA, Mbunge wao wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo ataenda kwenye eneo la ujenzi KUPIGA HARAMBEE.
Vilevile Wananchi wamesisitiziwa umuhimu wa kuendelea kuboresha Miundombinu ya Elimu kwenye Shule zao za Msingi na hiyo Sekondari ya Kata.
MWAKA HUU MPYA (2019) NI MWAKA WA VITENDO – KINACHOHITAJIKA NI UTEKELEZAJI WA MIRADI KWA VITENDO.