AFYA BORA MUSOMA VIJIJINI – DARUBINI (MICROSCOPES) 2 ZATOLEWA

Uhuru Hospital ya Mwanza imetoa DARUBINI MPYA 2 zitumiwe Jimboni. Dr Derick Davis Nyasebwa, Kiongozi wa Uhuru Hospital na mzaliwa wa Kijiji cha Rusoli, Musoma Vijijini amemtaarifu Mbunge wa Musoma Vijijini kwamba DARUBINI hizo zikachuliwe Mwanza siku ya Jumatatu, tarehe 19.3.2018. Wananchi Jimboni wanaendelea kujenga Zahanati (vijijini, jumla 68) na Vituo vya Afya (Kata, jumla 21). Wasomi, Wataalamu na Wafanya biashara wanaofanya kazi zao ndani na nje ya Jimbo wameamua kushirikiana na ndugu zao vijijini kwenye miradi ya ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya elimu na afya Jimboni. JITOKEZE, TUTOKOMEZE UMASKINI JIMBONI MWETU.

Ofisi ya Mbunge