MBUNGE WA JIMBO ANUNUA TRACK SUITS 100 NA JEZI 16 KWA AJILI YA TIMU YA UMITASHUMTA YA MUSOMA VIJIJINI

Timu ya UMITASHUMTA ya wanafunzi wa Shule za Msingi za Musoma Vijijini wako kambini wakifanya mazoezi yakiwa ni kwa ajili ya maandalizi yao ya mashindano ya UMITASHUMTA Mkoa wa Mara.

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo amechangia ushiriki wa wanafunzi wetu kwenye mashindano hayo kwa kununua:
*Track suits 100
*Jezi 16 za wachezaji wa mpira wa miguu

Picha za hapa zinaonesha:
Wanafunzi wakiwa mazoezini kwenye Shule ya Msingi Suguti, Kijijini Suguti, Kata ya Suguti

Michezo na Utamaduni:
Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020-2025 inaelezea umuhimu wa michezo na utamaduni kwa Taifa letu.

Michezo na Utamaduni ni moja ya vipaumbele vikuu vitano (5) vya Jimbo letu, na inatekelezwa vizuri.

Tunawatakiwa wanafunzi wetu ushindi mzuri kwenye mashindano ya UMITASHUMTA

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Tarehe:
Jumapili, 26.5.2024