MRADI WA UMWAGILIAJI WA BUGWEMA KUKABIDHIWA MKANDARASI MWEZI HUU

Taarifa mpya (update):
Bonde la Bugwema, Musoma Vijijini

MRADI WA UMWAGILIAJI WA BUGWEMA KUKABIDHIWA MKANDARASI MWEZI HUU

Tarehe ya tukio:
Jumamosi, 18.4.2026

Muda: Saa 4 asubuhi

Mahali:
Kijijini Bugwema
Kata ya Bugwema

Jina la Mkandarasi:
China Railway Bureau Ltd

Gharama za mradi:
Tsh bilioni 48 (Tshs 48b)

Historia fupi ya Mradi:
Mradi huu ulianzishwa na Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1974.

Tarehe 6.2.2022, Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan aliombwa na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini afufue mradi huu - Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan akakubali na kuagiza Wizara ya Kilimo itekeleze uamuzi wake. Ahsante sana Mhe Rais, tunashukuru sana sana!

Matayarisho ya Mkandarasi kukabidhiwa mradi yanaendelea na taarifa zaidi zitatolewa.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6
Musoma

Date: Sat, 4 April 2026